NAY WA MITEGO NDANI YA SKENDO NZITO YA KUVUNJA PENZI LA ALLY TIMBULO KWA SKAINA -


 
Skyner Ally ‘Skaina’.
CHIPUKIZI wa Bongo Fleva, Ally Timbulo amefunguka kuwa alimwagana na mwigizaji Skyner Ally ‘Skaina’ kwani aligundua kuwa ana uhusiano na Mbongo Fleva mwenzake, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
‘Akikonfesi’ mbele ya kinasa sauti cha Ijumaa Wikienda, Timbulo alisema ishu hiyo ilitokea miaka kadhaa iliyopita ambapo ‘alimsarendia’ mlimbwende huyo ili awe mpenzi wake na aliposhtuka kuwa ana uhusiano na Nay wa Mitego, fasta alibadili uelekeo.
Ally Timbulo.
“Daah! Nilipogundua ana uhusiano na Nay, fasta nilimpotezea,” alisema Timbulo, alipotafutwa Skaina, alisema: “Usiniulize hizo habari, ulivyosikia ndiyo hivyohivyo.”

0 comments: